ASKOFU MKUU wa Jimbo Kuu Katoliki
SONGEA Mhashamu Damiani Denis Dallu amewataka Waamini, Mapadri pamoja na Watawa
kuwa na hofu ya Kimungu katika kutimiza wajibu wao na majukumu ya kila siku.
Askofu Mkuu DALLU ametoa wito huo katika mahubiri yake wakati wa Ibada Takatifu
ya kubariki mafuta matakatifu ibada, iliyofanyika katika Kanisa Kuu la Kiaskofu
Jimbo Kuu Katoliki SONGEA.
Amesema kuwa kukosekana kwa hofu ya
Mungu kulipelekea wana wa ISRAELI kuingia utumwani Babeli, ambapo yalikuwa
matokeo ya kumuasi Mungu, hivyo basi Mkristo yoyote yule anapaswa kuwa na hofu
ya Mungu wala si hofu ya kiutawala kama waliyokuwa nayo wana wa ISRAEL.
Akizungumzia Mafuta Matakatifu,
Askofu DALLU amesema tangu mwanzo kulikuwako na utaratibu wa kuweka Wakfu kwa
kuwapaka mafuta watu kama walivyofanyiwa Watawala na manabii, ambapo amewataka
Mapadri kuwa Watakatifu kama mafuta wanayoyabariki na kuyatumia katika
Sakramenti za Kanisa.
Askofu DALLU amehitimisha mahubiri
yake kwa kuwahimiza Mapadri wote kuzidisha juhudi katika kuchuchumilia
Utakatifu wakiwa na hofu ya Mungu ndani mwao, ili wanapotumia
mafuta hayo watu watakatifuzwe.

Comments
Post a Comment