Askofu wa Jimbo Katoliki MTWARA
Mhashamu TITUS MDOE, amewataka
Vijana wa Jimbo Katoliki MTWARA
pamoja na Vijana wengine wote kuwa na msimamo wa Kiimani kwa kumfuata
KRISTO na kuyafanya yanayopendeza katika jamii.
Askofu MDOE ametoa wito huo katika
homilia yake wakati akiadhimisha Ibada ya Misa Takatifu ya Dominika ya Matawi
iliyofanyika Parokia ya Kanisa Kuu parokia ya Watakatifu Wote Jimboni
MTWARA, ambapo ilienda sanjari na siku ya 33 ya Vijana Ulimwenguni.
Amesema kuwa, Vijana wanapaswa kujitambua
katika maisha yao wanayoishi, ikiwemo kumkumbatia KRISTO, kusimamia miongozo ya
Imani, kulitunza na kulipenda Kanisa, kwani pasipo kufanya hivyo watabaki
katika mahangaiko, huku wakikumbana na changamoto nyingi za kimaisha.
Aidha Askofu MDOE amewaomba Wazazi
na Walezi kuwa mstari wa mbele, katika suala zima la malezi kwa vijana wao, ili
kutengeneza jeshi imara lenye misingi bora ya kumjua na kumfuata KRISTO.

Comments
Post a Comment